Kiburi
ni hali au tabia ya kukosa unyenyekevu.
Dhambi hii humwingia mtu kwa
siri pasipo yeye kujua na inatenda kazi ndani yake. Mtu anapokuwa na
dhambi hii hufanyika kuwa chukizo kwa Bwana, Mith 16:5.
DALILI ZA KIBURI
1. Kujihesabu kuwa yeye ni safi, Luka 18:11.
2. Kutokubali udhaifu alio nao, Mwa 3:12.
3. Hakubali kufundishwa wala kujifunza, Isaya 26:10.
4. Kuona anajua mambo yote, 1Kor 8:2.
5. Hahitaji msaada wa neno la Mungu, Mith 21:24.
6. Kutokutetemeka asikiapo neno la Mungu, Isa 66:2b.
7. Huona vigumu kumtii mwenye mamlaka, Rum 13:2.
8. Huona hawezi kujishughulisha na mambo manyonge, Rum 12:16.
9. Humzoea kiongozi wake wa kiroho, hudharau maonyo na hukosa hofu ya Mungu moyoni mwake, Mith
10:17.
10. Hujivunia vipawa vyake, Luka 18:11.
HASARA ZA KIBURI
1. Kupata maangamivu, Mith 16:18.
2. Bwana kung'oa nyumba yake, Mith 15:25.
3. Sala zake ni chukizo, Mith 28:9.
4. Kushushwa na kuinamishwa, Mith 29:23; Lk 14:11; Mt 23:12; Yer 49:16; Isa 2:11,12.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni