Gal
5:25
i.
Kutembea katika Roho ni kutekeleza maamuzi ya
Roho na kuishi ndani ya mwongozo wake na si kuenenda au kuingiza au kujaribu
kurekebisha au kubadilisha mwongozo.
ii. Kutembea
katika Roho ni kufanya mambo yale ambayo torati na mwili vimeshindwa kuyafanya.
MAMBO
YA KUZINGATIA KATIKA KUTEMBEA KATIKA ROHO
1. UJUE
UDHAIFU WAKO, Yak 3:2
Jambo hili ni la muhimu sana na kamwe
halipaswi kupuuzwa. Unatakiwa kuubaini udhaifu wako kwa sababu kweli iliyomo
ndani yako ni adui na inaujua udhaifu wako kuliko wewe. Lielewe eneo hili kwa
makini na umkabidhi Roho Mtakatifu ambaye ni rafiki mwema na mnasihi wa milele naye
atakutia nguvu na kukusaidia kuutambua na kuzuia majaribu na vishawishi.
2. YAFISHE
MATENDO YA MWILI KWA ROHO, Rum 8:3
Mtu ambaye amefanywa upya na Roho hawezi
kunaswa katika dhambi. Kwa Roho, tamaa za mwili zinashindwa. Kuyafisha matendo
ya mwili ni adhimu ni sawa na kusema “dhambi hapana” lakini ni tofauti na
kampeni ya kupambana na madawa ya kulevya miongoni mwa vijana miaka mingi
iliyopita. Kusema “dhambi hapana” pekee haitafanikiwa, kusema “dhambi hapana” kamwe huwezi ukashinda dhambi. Je
nini unatakiwa ufanye? Sema “hapana Kwa Roho.
3. UONGOZWE
NA ROHO, Rum 8:14; Efe 5:15
Roho mtakatifu hutuongoza wakati wote.
Hutuongoza kupitia neno lake lililofunuliwa kwa manabii, 2Pet 1:20, 21.
Tunapaswa kuwa waangalifu, waombaji na wanyenyekevu katika kutumia hekima pana
ya Biblia katika hali tunazokutana nazo. Wakati mwingine Roho Mtakatifu hutuongoza
moja kwa moja. Roho Mtakatifu anaweza kutenda kwa njia yoyote, kulingana ratiba
yoyote kama apendavyo. Hatumwongozi namna au wakati gani atembee. Biblia
imebainisha mifano mingi ya jinsi Roho Mtakatifu anavyoweza kutenda, tunapaswa
kukubali kuwa wakati mwingine aweza kuchagua kutuongoza moja kwa moja kama
tutakuwa huru na tu katika mwongozo wake.
4. UJUE
U BABA WA MUNGU KWA ROHO Rum 8:15-17
Pasipo Roho Mtakatifu tusingeujua
utambulisho wetu kuwa tu wana wa Mungu. Ashukuriwe Mungu aliyetupatia Roho
Mtakatifu bure, na mistari hii kutoka Rum 8 inaonesha mambo matatu ya ajabu
ambayo Roho Mtakatifu ameyafanya:
a. Anatenda
kama kiunganishi ambaye ametutoa mahali pa utumwa na hofu na kutuleta mahali pa
kupitishwa na kukubaliwa.
b. Anatusaidia
kulia “ABBA” yaani baba.
c. Anashuhudia
na roho zetu kuwa tu wana wa Mungu.
5. OMBA
KATIKA ROHO, Rum 8:26-28
Mistari hii miwili (Rum 8:26,27) ina utajiri mwingi na inatusaidia katika
kuishi kwetu katika Roho.
a. Tunajifunza
kuwa tu dhaifu tunapokuwa katika kuomba. Hatujui kuomba katika hali yoyote.
b. Tunajifunza
kuwa Roho huungana kutusaidia tunapotaka kujua jinsi ya kuomba kwa ktuombea kwa
kuugua kusikoweza kutamkwa.
c. Roho
huchunguza mioyo yetu na kujua akili zetu kwamba zimeelekezwa kwake hata kama
hatujui namna ya kuomba.
d. Matokeo
ni kwamba maombi yetu yanaomba “kulingana na mapenzi na Mungu” kwa sababu Roho Mtakatifu (anatembea katikati
yetu) anatuongoza kuomba na kuyawasilisha maombi yetu kwa baba.
FAIDA
ZA KUTEMBEA KATIKA ROHO
1. Kuwekwa
huru mbali na sheria ya dhambi na mauti, Rum 8:2-4.
2. Kuwa
hekalu la Roho Mtakatifu, 1Kor 6:19.
3. Kuyajua
mafumbo ya Mungu, 1Kor 2:10-15.
4. Kushirikishwa
uzima wa milele, Yn 3:5; Efe 2:5.
5. Kuongozwa
na roho, Lk 2:25, 26; Mdo 13:4, 16:6-10.
6. Kuthibitishwa
kuwa wana wa Mungu, Rum 8:16.
7. Roho
Mtakatifu kusema nasi, Mdo 10:19.
8. Kuwa
mashahidi, Mdo 5:32; Yn: 16, 17.